• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

MGOGORO MRADI WA MAJI, KIHANJU WAPATA MWAROBAINI

Posted on: March 18th, 2022

                     

Kikundi cha umoja wa Wajasiriamali Tarafa ya Itigi (UWATI) kimekubali kushirikiana na Wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) kutekeleza mradi wa maji katika kijiji cha Kihanju,Halmashauri ya Itigi kwa lengo la kutatua kero ya uhaba wa maji kwa matumizi ya kawaida pamoja na kilimo cha umwagiliaji.

Makubaliano hayo yamefikiwa katika kikao cha maridhiano  baina ya pande hizo mbili  kilicho fanyika katika Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Itigi baada ya kikundi cha UMATI  kudai kuwa RUWASA wamewanyang’anya mradi  walioumba kufadhiliwa na kampuni ya vinywaji ya  Serengeti (SBL) kwa lengo la kikundi hicho kufanya kilimo cha umwagiliaji cha zao la vitunguu.

Akitoa taarifa ya mradi  Eng. Maduhu kutoka RUWASA  wilaya ya Manyoni ameeleza kuwa mradi huo uliibuliwa na kikundi cha UMATI mwaka 2021 na kuandika andiko la kuomba msaada wa kujengewa miundombinu ya umwagiliaji pamoja na kisima katika eneo la mradi wao wa kilimo cha umwagiliaji  ambapa Kampuni ya vinywaji ya Serengeti(SBL) lilikubali kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni mia mbili(Tsh mil.200) kupitia Shirika la WaterAid Tanzania ili kutekeleza mradi huo

Aidha baada ya upembuzi yakinifu WaterAid,RUWASA mkoa Singida  na wilaya ya Manyoni pamoja na wadau mbalimbali wa maji walibaini uhaba wa maji kwa wakaazi wa Kihanju na kuamua kutoa kipaembele kwa wananchi kama sera ya maji ya mwaka 2002 inavyoelekeza ambapo jambo hilo liliibua hisia tafauti kwa kikundi cha UMATI .

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Mipango na Usimamizi  wa Miradi ya WaterAid Tanzania  Dkt.Nduhura Innocent ameishauri serikali  kupitia Halmashauri kutoa elimu kwa wana kikundi cha UMATI  kuelewa faida ya mradi huo kwa  jamii badala ya kuibua migogoro inayoweza kupelekea wadau kushindwa  kufadhili miradi mingine katika Halmashauri ya Itigi.

Naye Mjumbe wa UMATI Bw. Omari Malele amesema kuwa  kikundi kimeridhia mradi uendelee lakini kuwepo na ushirikishwaji  kwa kuwa kikundi hicho ndio kilichoibua huo mradi huku Kaimu Katibu wa UMATI Bw.Hamisi Samade  amewashukuru wajumbe kutoka WaterAid kwa kuja kutatua mgogoro uliokuwepo baina ya pande hizo mbili.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Itigi Mh. Hussein Simba akafafanua jinsi mchakato mzima wa uanzishwaji wa mradi ulivyokua shirikishi na kusema kuwa jamii  pamoja na kikundi cha UMATI wanapaswa kuchangia huduma ya maji  ili mradi huo uweze kujiendesha.

Usanifu wa Mradi wa maji wa Kihanju ulianza mwezi julai ,2021 na utekelezaji wake ukaanza mnamo Disemba 2021 na unatarajiwa kutosheleza mahitaji ya maji ya watu zaidi ya 2000 katika kijiji hicho na maeneo ya jirani.

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.