• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

Migogoro ya Wakulima na Wafugaji Wilayani Manyoni yapatiwa mwarobaini

Posted on: October 6th, 2017



MKUU WA WILAYA AKEMEA VIKALI VIASHIRIA VYA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI ITIGI


Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mkoani Singida ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu amekemea vikali viashiria vya mgogoro kati ya wakulima na wafugaji katika maeneo ya malisho na mashamba vinavyoanza kuchipuka na kuibua hisia za sintofahamu.


Migogoro ya wakulima na wafugaji huanza kwa majibizano ya mara kwa mara kati ya wananchi wenyewe kwa kuingiliana katika maeneo yao jambo ambalo likipuuzwa ingali dogo hukomaa na kupelekea serikali kutumia nguvu nyingi katika kulimaliza.


Akizungumza na wakulima na wafugaji kwenye ziara ya kikazi katika vijiji korofi vinavyochagiza mgogoro huo Mhe Miraji Jumanne Mtaturu aliwataka wananchi kuacha haraka kuibua hasira baina yao jambo ambalo linawezekana kutatulika.


Aliwataka wakulima ambao wamevamia katika maeneo yaliyohifadhiwa kwa ajili ya mpango wa matumizi bora ya ardhi kuondoka haraka katika maeneo hayo na kutafuta maeneo mengine kwa ajili ya kilimo kwani endapo kama watakiuka maelekezo hayo serikali itachukua hatua dhidi yao.


Aliwataka wakulima hao waliovamia maeneo hayo kufika ofisi ya Afisa Mtendaji wa kijiji ili kubaini kama wanastahili kupatiwa maeneo mengine kutokana na kukutwa katika maeneo hayo mara baada ya kuanzishwa sheria ya matumizi bora ya ardhi ya mwaka 2007.


Mhe Mtaturu alisema kuwa Mgogoro wa kimaeneo ya malisho na mashamba ambao umeanza kumea katika kipindi cha hivi karibuni Wilayani Manyoni unahusisha Vijiji jirani vya Itigi Mjini, Doroto na Damwelu vinavyochangia maeneo hayo.


Alisema kuwa ni lazima kila mwananchi kuwa wakala wa kuhifadhi na kutunza mazingira katika maneo yanayotuzunguka ikiwa ni pamoja na kutolima katika maeneo ambayo yamehifadhiwa au kupangwa kwa ajili ya mambo mengine.


Hata hivyo alimuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi kufatilia ili kubaini aliyetoa maeneo ya wafugaji kwa wakulima ili achukuliwe hatua za kisheria kwani jambo hilo lina dalili zote za rushwa na uhujumu wa maeneo.


Sambamba na hayo pia Kaimu Mkuu huyo wa Wilaya ya Manyoni ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu aliwataka wananchi kuelekea msimu wa kulima mazao ya kipaumbele ambayo ni Pamba, Korosho, Chai, Kahawa na Tumbaku.


Aidha, alisema kuwa pamoja na mazao hayo ya kipaombele lakini wanapaswa kuongeza kasi katika kilimo cha mazao ya chakula na Biashara hususani mahindi, mtama, Dengu na zao la Alizeti.


Aidha, Mhe Mtaturu aliwashauri  wafugaji kupunguza idadi ya mifugo waliyonayo kwa kuuza na kununua au kujenga nyumba za kuishi ikiwa ni njia mojawapo ya kuweza kukidhi maeneo ya malisho yaliyopo.

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.