• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

NITASHUGHULIKIA MALALAMIKO YA AJIRA SGR-DC,MANYONI

Posted on: November 12th, 2022

Mkuu wa wilaya ya Manyoni  Bi.Rahabu Mwagisa amesema atafuatilia kwa makini utaratibu unaotumika kutoa ajira  katika mradi wa ujenzi wa reli ya treni ya mwendokasi kutoka na kuwepo kwa malalamiko mengi kutoka kwa wananchi.

Akizungumza na wakazi wa Mji wa Itigi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Songambele,kata ya Tambukareli Mkuu huyo wa Wilaya ya Manyoni amesema mradi wa SGR unatarajia kutoa nafasi za ajira takribani mia tano kwa Wilaya ya Manyoni na kwamba ajira hizo zitatolewa kwa awamu.

Baada ya kusikiliza kero na maoni mbalimbali kutoka kwa wananchi waliofika katika mkutano huo  Mwagisa amesema kuwa amepokea meseji nyingi za malalamiko kutoka kwa wananchi juu ya namna ajira hizo zinavyotolewa na kupelekea wananchi kukosa imani na mchakato mzima wa zoezi hilo.

Amebainisha kuwa utaratibu wa ajira ulivyo katika mradi huo ni kwamba wananchi katika maeneo yanayopitiwa na mradi wanapaswa kupewa kipaumbele lakini amekuwa akipokea malalamiko kuwa wanao ajiriwa ni wageni kutoka nje ya maeneo mradi ukakopitia.

Mkuu huyo wa Wilaya amesema amesema atakutana uongozi wa Kampuni ya Yapi Markez  inayotekeleza mradi wa SGR ili kuzungumzia suala hilo .

‘’Nitakutana na Waturuki nifanye nao mkutano nadhani kuanzia wiki ijayo ili tuweze kubaini tatizo lilipo, kama ni wao au kuna watu wanatumika tuweze kudili nao’’alisema Mwagisa

Baadhi ya wananchi waliozungumzia suala hilo mbele ya Mkuu wa wilaya aliye ambatana na timu yake ya wataalamu kutoka Manyoni pamoja na halmashauri ya Itigi ni pamoja na Bwana Mayoi Elieza,Hamisi Samade na Yussuf Muhuta wamebainisha changamoto za mchakato wa upatikanaji wa ajira katika mradi wa SGR ni pamoja na umbali wa mahali/ kituo cha kufanyia usaili ambapo kwa sasa wanalazimika kwenda Tabora,pamoja na kuwepo kwa viashiria vya rushwa na kumuomba Mkuu wa wilaya kuwasaidia ili anayestahili kupata ajira  apate.

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.