• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Itigi District Council
Itigi District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
      • Maji
      • Afya
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Mji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Shera Ndogo
    • Fomu za maombi Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Taarifa kwa umma

Chuo cha Veta Manyoni Kujengwa Makao Makuu ya Wilaya- RC Serukamba

Tarehe ya Kuwekwa: April 5th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba leo tarehe 5 Aprili, 2023 amemaliza mgogoro wa eneo kitakapojengwa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kwa kufikia maamuzi kwamba chuo hicho kujengwa katika eneo la Manyoni Makao makuu ya Wilaya.


Maamuzi hayo ameyatoa katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni na kuwakutanisha wenyeviti wa Halmashauri zote za Wilaya hiyo, Wabunge wa Manyoni, Madiwani wa Halmashauri ya Itigi na Manyoni, Kamati ya Siasa ya Wilaya na ya Mkoa na Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya na mkoa.


RC Serukamba alipitisha uamuzi wa Chuo hicho kujengewa katika eneo la Setelite Manyoni karibu na eneo la mnada baada ya kuwahoji Madiwani wa upande wa Manyoni na Itigi na kubaini kwamba hapakuwa na ushirikishwaji katika upatikanaji wa eneo lililopendekezwa mwanzoni ambalo ni Kintiku Lusilile.


Madiwani pamoja na Wabunge walilazimika kupiga kura ya wazi kwamba ili kuamua chuo hicho kujengewa wapi kati ya Kintinku, Lusilile au Manyoni Setalite ambapo kura 10 zilitaka kijengwe Lusilile, 4 zilitaka kijengwe Itigi na kura 32 zilitaka kijengwe Manyoni.


Aidha Serukamba alieleza kwamba eneo hilo lipo katikati hivyo ni rahisi kufikiwa na wananchi wa maeneo yote ya Wilaya hiyo,

"Maoni ya wengi ni Maoni ya Mungu kwa kuwa wengi wameona chuo hicho kijengwe Manyoni lazima tufanye hivyo ili kiweze kuwasaidia wananchi kutoka pande zote, na wote naomba tuweze kusimamia hili," Alisema Serukamba


Hata hivyo amemuagiza Mkuu wa Wilaya hiyo kuhakikisha eneo hilo linapimwa na wakabidhiwe Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati kwa ajili ya kuanza hatua za Ujenzi.


Hata hivyo amewataka Viongozi wa Wilaya hiyo kuandaa ziara katika kata zilipotakiwa kujengwa chuo hicho na kuwaelimisha sababu za msingi za kuhamishwa ujenzi huo.



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI ZA MKATABA October 17, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI ZA MKATABA October 17, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA April 08, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MAADHIMISHO SIKU YA UKIMWI

    December 10, 2024
  • SITAKI KUONA MTU ANACHEZA NA WATOTO WA SHULE-RC DENDEGO

    November 10, 2024
  • DC MANYONI APIGA MARUFUKU UKATAJI WA VICHAKA VYA ITIGI

    November 01, 2024
  • SERIKALI KUBORESHA HALI YA WAZEE

    October 17, 2024
  • Tazama zote

Video

WALIOFAULU WARIPOTI SHULENI
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Hotuba mbalimbali
  • Taarifa mbalimbali

Tuvoti mashuhuri

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

Kinasajii Watumiaji Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watumiaji

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Itigi

    Anwani ya Posta: S. L. P. 70 Itigi

    Simu: 0684483226

    Simu ya Mkononi: 0684483226

    Barua pepe: ded.itigidc@singida.go.tz

Mawasiliano Yetu

   

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • MMM
    • Ramani

Haki miliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Itigi :Haki zote zimehifadhiwa