• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

DC.LWOTA AZINDUA ZAHANATI KITONGOJI CHA IKANAMALENGA

Posted on: August 24th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Kerembe Lwota amezindua Zahanati ya kata ya Ipande ambapo amesema ameridhishwa na jitihada za wananchi katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi huo iliyojengwa kwa nguvu za wananchi  pamoja na  fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri hadi kukamilika .

Akizungumza na wananchi wa kitongoji cha Ikanamalenga katika uzinduzi huo, DC.Lwota amesema amewapongeza wananchi hao kwa juhudi zao katika shughuli za maendeleo hususani ushiriki wa wananchi katika ujenzi wa zahanati hiyo

Amesema kutokana juhudi na utayari wa wananchi serikali inayoongozwa na Mhe,Dkt Samia Suluhu Hassani,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitoa shilingi milioni hamsini(Mil.50) ili kuhakikisha zahanati hiyo inakamilika na huduma za kiafya zinaanza kutolewa.

“Nimeambiwa kuna maeneo walianza mradi miaka mitatu nyuma na haijakamilika lakini hapa mmefaulu licha ya changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa maji, nawapongeza sana ”alisema, DC Lwota

 Aidha DC ametoa rai kwa wananchi kutunza mradi huo muhimu pamoja na kuwapa ushirikianao watumishi waliopangiwa kutoa  huduma za afya  katika zahanati hiyo ili waweze kutoa huduma stahiki kwa jamii.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi Dkt.Emmanuel Mallange kwa niaba ya Mkurugenzi wa halmashauri amesema Wananchi walionesha jitihada kubwa kwa kujitolea kujenga  zahanati hiyo kufikia hatua ya lenta ndipo serikali kupitia mapato ya ndani ya halmashauri ikatoa kiasi cha shilingi milioni hamsini (Tshs 50,000 000/= ) ili kukamilsha mradi huo.

 Naye, Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Manyoni Ndg. Jumanne Ismail Makanda amewataka wakazi wa Kata ya Ipande hususani akina mama kuitumia vizuri zahanati hiyo kwa kwenda kupata huduma kwa wakati.

“ Itakua ajabu kuona akina mama wajawazito wanajifungulia nyumbani na kujiweka katika hatari zinazotokana na changamoto za uzazi wakati serikali imewasogezea huduma katika maeneo yao “alisisitiza

Pia Diwani wa Kata ya Ipande  Mhe. Kedmond Mpondo amebainisha kuwa wazo la ujenzi wa zahanati lilitokana na mkutano wa wananchi walipokubaliana kujenga zahanati kama  kipaumbele kati ya mahitaji waliyo nayo.

“Mwaka jana [2022]  tulifanya kikao na wananchi na tukakubaliana kuwa tujenge zahanati kwa kujitolea nguvu zetu na ndipo serikali ikatuunga mkono katika hatua ya ukamilishaji”alifafanua  Mhe Mpondo

Mhe.Mpondo amewapongeza wananchi kwa kushiriki ipasavyo katika mradi huo licha Kitongoji hicho kuwa na changamoto kubwa ya uptikanaji wa maji .

Katika ziara hiyo Mkuu wa Wilaya alitembelea Shule Shikizi ya Katumba,Zahanati ya Mkajenga pamoja na kufanya mkutano wa hadhara na wananchi katika kitongoji cha Mkajenga.

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.