• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

KAMPENI"ONJAMA" KUIOKOA MANYONI NA BAA LA NJAA

Posted on: April 8th, 2023

Halmashauri ya  Wilaya ya Manyoni imekuja na mpango wa  kutokomeza baa la  njaa katika Wilaya hiyo kwa  kuibua Kampeni ya Ondoa  Njaa Manyoni (ONJAMA) kwa kuhamasisha wananchi kulima mazao yanayostahimili ukame  kulingana na jografia ya eneo hilo.

Akizungumza katika Kikao cha Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Itigi Mkuu wa Wilaya ya Manyon Mhe.Kemilembe Lwota amesema  serikali imekuwa ikifanya kazi nzuri ya kuwapatia wananchi chakula cha bei nafuu katika maeneo yenye njaa ikiwemo wilaya ya Manyoni lakini amesisitiza kuwa utaratibu huo wa kutegemea serikali kuwapatia chakula ufike kikomo.

Amesema  pamoja na jografia ya Wilaya hiyo kuwa na mvua zisizotabirika  bado wananchi wanaweza kulima mazao ya chakula kama mihogo,mtama,uwele na mazao mengine ambayo yanaweza kuhimili mvua chache huku akiwataka madiwani kwenda kuhamasisha wananchi katika maeneo yao kulima mazao ya aina hiyo ili kuepuka  baa la njaa kujirudia katika wilaya hiyo.

Kwa upande mwingine DC.Lwota amewataka Madiwani, Divisheni ya Elimu na viongozi wa ngazi ya Kata kuhakikisha wanafunzi wote wanaotakiwa kuwa shuleni katika hatua ya elimu msingi na sekondari kuripoti shuleni mara tu shule zitakapofunguliwa.

Amesisitiza kuwa serikali imefanaya kazi kubwa ya kujenga miundombinu bora ya elimu ikiwemo vyumba bora na vya kutosha vya madarasa lakini changamoto imebaki katika zoezi la uandikishaji wa wanafunzi na kusema kuwa jambo hilo halikubaliki.

Awali akifungua kikao hicho Mwenyekiti wa Halmashauri ya Itigi Mhe. Hussein Simba amebainisha kuwa halmashauri hiyo kwa kiwango kikubwa inategemea makusanyo yanayotokana na mazao ya kilimo ambapo kufikia sasa makusanyo ya halmashauri ni takribani milioni 894 ikiwa ni sawa na  asilimia 47.

Mhe.Simba amebainisha mikakati ya kuongeza nyanzo vingine vya mapato ikiwa ni pamoja na kujenga maegesho ya maroli na stendi ya magari katika mji wa Itigi na stendi ya magari katika  kata ya Rungwa ambayo ujenzi wake unaendelea  kufikia sasa kwa gharama ya shilingi milioni thelathini huku akishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais,Dkt Samia Suluhu Hassani kwa kuendelea kutekeleza miradi mikubwa  ya kimkakati Ili kutoa huduma kwa wananchi.

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.