• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

MGANGA MKUU ITIGI DR MALLANGE AENDELEZA OPERATION FUNGIA MAABARA BUBU

Posted on: February 4th, 2020

Dr Emmanuel mallange ambaye ni mganga mkuu katika halmashauri ya Wilaya ya Itigi ameendelea na operation   ya kufungia maabara bubu ambazo zinatoa huduma za upimaji wa magonjwa katika kata na vijiji mbalimbali katika halmashauri ya itigi

Dr mallange akiwa na Timu ya ukaguzi   walifika katika kata ya ipande  katika  halmashauri ya wilaya ya Itigi wakiwa katika ukaguzi wa kawaida na kupata habari  kwa wananchi kuwa kuna Maabara ipo katika kata ya ipande kitongoji cha mngalalee  ambayo inatoa huduma za upimaji pamoja na huduma za uzalishaji ambapo inasadikika akina mama wawili wamejifungulia katika maabara hiyo bubu nyakati za usiku.

Baada ya kupata habari hiyo Dr Mallange na Timu yake walifika katika maabara hiyo na kukuta baadhi ya wagonjwa wakiwa wanasubiri kupata huduma za vipimo pamoja na kuandikiwa dawa ili wakanunue kwenye duka bubu ambalo halina usajili lililopo pembezoni mwa Maabara hiyo isiyokuwa na jina.

Muhudumu wa maabara hiyo bubu ambaye alifahamika kwa jina Moja la bwana Gasper alifanikiwa kukimbia baada ya kuona maafisa wa ukaguzi wanafika katika maabara hiyo. Hata hivyo Dr Mallange aliwachukua wagonjwa wote waliokuwa wanasubiri huduma katika maabara hiyo na kuwapeleka katika zahanati ya Ipande na kupatiwa matibabu ipasavyo. Pamoja na Mhuhudumu huyo kukimbia Dr Mallange amemtaka mmiliki wa nyumba hizo zinazoendelesha Maabara na Duka bubu bwana Robart Chalamaganza kufika Ofisini kwake haraka iwezakanavyo vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Aidha   Dr Mallange alitumia fursa hiyo kuwaelimisha wananchi na wagonjwa hao umuhimu wa kujiunga na Mfumo wa bima ya Afya ya jamii iliyoboreshwa ambapo wanachi hao waliona unafuu ni mkubwa sana kwao kwa kuwa na bima ambayo wanaweza kutibiwa kuanzia ngazi ya zahanati mpaka hospitali ya Mkoa na kuomba Afisa Muandikishaji awatembelee katika kaya zao ili waweze kuijunga na Mfuko huo ambao una faida kubwa sana katika kupata matibabu yenye unafuu.

Hata hivyo dr Mallange amewashukuru wananchi kwa kutoa taarifa za kutoridhishwa na utoaji huduma wa maabara na maduka bubu ambayo yanafanya kazi katika kata hiyo ya ipande

Aidha Timu hiyo ya ukaguzi imefungia maduka ya madawa   mawili bubu ambayo yanamilikiwa na bwana Robert Chalamaganza  pamoja na bwana Hamisi Abasi pamoja na kuchukua dawa zote pamoja na vifaa vyote vilivyokuwemo  katika maabara bubu. Kwa upande wake Mratibu wa Maabara wilaya Bi Pendo Kiula amesema kuwa uamuzi wa uchukuaji wa vifaa hivyo vya maabara unatokana na Maabara hiyo bubu kutokidhi hata kitu kimoja kati ya vigezo vinavyotakiwa katika ufunguaji wa maabara  ikiwemo Jina la maabara ,Aina ya Maabara ,Kibali /kuandikishwa ,Wafanyakazi wenye sifa ,Majengo/jengo n.k

Naye Petro Loya(39) mkazi wa kata ya ipande kitongoji cha msumbiji ambaye alikuwa na mgonjwa wake Jonas Julius (14) wameishukuru sana serikali kwa kufuatilia maabara hizo ambazo wakati mwingine wanakwenda kwa kupotoshwa kuwa Hospitali za serikali hazina dawa. Bwana Loya amesema kuwa mgonjwa wake baada ya kumpeleka zahanati ya ipande  amepata huduma nzuri za vipimo pamoja na kupewa dawa ambazo hakutegemea kama angeweza kuzipata.

Aidha bwana loya ameishukuru sana serikali kwa uanzishwaji wa mfuko wa bima ya Afya ya jamii kwa kuwa imemfanya mgonjwa wake atibiwe kwa gharama ndogo sana kuliko ambako angetoa fedha hizo kwenye maabara bubu ambako huwa anatumia kiasi cha sh 40,000 mpaka sh 30,000 kila wakati anapokwenda kwenye maaabara hizo. Pamoja na hivyo bwana  Loya amewaomba wanachi ambao hawajajiunga na Mfuko wa bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa wajiunge sasa kwa kuwa Ndio Mkombozi wao kwa kupata Huduma bora za Matibabu.

Jengo la Maabara Bubu inayotumika katika kijiji cha ipande lenye Mlango wenye geti jekundu na kiti cha kukalia wagonjwa (kushoto)Pamoja na Mlango wenye geti jekundu na Kiti cha kukalia wateja (kulia ) ambapo duka la madawa bubu ndipo ninapofanyia kazi

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya Itigi Dr Emanuel Mallange (Kushoto) akiwa na Wagonjwa ambao wanasuburi kupata huduma  kwa kificho katika Nyumba ya bwana Robert Chalamaganza baada ya kuona timu ya Ukaguzi imefika katika Eneo hilo.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya Itigi Dr Emanuel Mallange (katikati) Akitoa Msaada wa Kupakia wagonjwa ambao walikuwa hawajiwezi kwenye gari na Kupelekwa katika Zahanati ya Ipande kwa matibabu zaidi

Mratibu wa Maabara wilaya Bi Pendo Kiula(Kulia ) Pamoja na Mganga Mkuu (Kushoto) wakiangalia vifaa vilivyokutwa kwenye maabara Bubu iliyopo katika Kijiji cha Ipande katika Halmashauri ya Itigi

 Mganga Mkuu Dr Mallange Akiwafuatilia Wagonjwa kwa Usafiri wa Baiskeli wagonjwa baada ya Wagonjwa Hao kupelekwa katika Zahanati ya Ipande.

Mganga Mkuu Dr Mallange (kushoto) akiwa na bwana Petro Loya ambae amehamasishwa Umuhimu wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii iliyobreshwa na kupelekea kujiunga na siku hiyo hiyo kwa sh 30000 .

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.