• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA WAKUU WA MIKOA NA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA

Posted on: July 28th, 2022


Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa wakuu wa mikoa wapya, kuwahamisha vituo vya kazi waliokuwepo, huku akiwatema tisa akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Ally Hapi.

Uteuzi huo umetangaza leo Alhamisi Julai 28, 2022 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura Yunus

Taarifa hiyo imewataja wakuu wa mikoa wapya ni aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido mkoani Arusha, Nurdin Babu ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Fatma Mwasa ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.

Rais Samia pia amemteua Halima Dendego kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk Raphael Chegeni ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Peter Serukamba ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Pia Rais amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, mkoani Pwani, Kanali Ahmed Ahmed kuwa Mkuu wa Mkoa Mtwara, aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, Kanali Laban Thomas ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

Taarifa hiyo imeeleza Rais Samia amemteua Albert Chalamila kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Dk Yahaya Nawanda ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.

Waliohamishwa

Taarifa hiyo imeeleza wakuu wa mikoa waliohamishwa vitu vya kazi ni aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthon Mtaka amehamishwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Queen Sendiga amehamishwa kuwa Mkuu wa Mkoa Rukwa.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Waziri Kindamba amehamishwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, pia aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Martin Shigella amehamishwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Omary Mgumba amehamishwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Adam Malima amehamishwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule amehamishwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Wanaoendelea na vitu vya kazi

Taarifa hiyo pia imeeleza kuwa Rais Samia amewabakiza wakuu wa mikoa 10 kubaki kwenye vituo vyao vya kazi akiwemo Amos Makalla Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Charles Makongoro Nyerere, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Sophia Mjema, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Batilda Burian na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge.

Wakuu wa mikoa walioachwa

Rais Samia amewatema wakuu wa mikoa tisa akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Ally Hapi, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, David Kafulila.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Robert Gabriel, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Brigedia Jenerali Marco Gaguti, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Charles Mbuge, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk Binilith Mahenge na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Joseph Mkirikiti

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.