• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

RAIS SAMIA AMWAGA BIL 1.6/- KUTEKELEZA MIRADI ITIGI

Posted on: November 1st, 2023

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan amekabidhi takribani Sh.Bilioni 1.6 kwa ajili ya kukamilisha miradi ya sekta ya afya na elimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida.

Hayo yamebainishwa Oktoba 31, 2023 kupitia kikao cha robo ya kwanza cha Baraza la madiwani cha kujadili mambo mbalimbali ambacho kilikuwa na ajenda nane.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo. Hussein Simba alisema kati ya fedha hizo Sh. Milioni 700 zitatumika kununua vifaa tiba.

Alisema fedha nyingine Sh.Milioni 100 zinakwenda kujenga zahanati mbili na hivyo kuongeza idadi ya ujenzi wa zahanati hizo kufikia nane na kuwa Sh.Milioni 500 zitatumika kujenga jengo la kufulia, jengo la mionzi na dawa katika Hospitali ya Wilaya.

Simba aliongeza kuwa Sh.Milioni 180 zitatumika kwa ajili ya kuziboresha shule 10 kongwe na Sh.Milioni 128 zinakwenda kujenga bweni kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalumu.

Alisema Sh.Milioni 544 zinakwenda kujenga Shule ya Sekondari ya Majengo na zitakazosalia zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa matundu 20 ya vyoo. 

Aidha, Simba alisisitiza kwamba halmashauri hiyo imekuwa ikikusanya mara dufu zaidi ya mapato ikilinganishwa na awali ambapo mpaka sasa kiasi kilicho kusanywa kinafikia asilimia 54 na kuwa matarajio yao hadi itakapofikia robo ya tatu watafikisha asilimia 100.

Simba alipongeza juhudi za Serikali kupitia Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan namna ambayo imeonesha ushirikiano uliotukuka kwa halmashauri hiyo katika muktadha chanya wa ustawi wa maendeleo ya watu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Leila Sawe na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa wilaya hiyo, Jumanne Ismail walisisitiza halmashauri hiyo kusimamia ipasavyo matumizi ya fedha zote zinazotolewa na Serikali na wadau mbalimbali wa maendeleo.

 Naye Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, John Mgalula akizungumza kwenye kikao hicho alipokea ombi la Diwani wa Kata ya Rungwa, Said Yahaya ambaye aliomba asilimia 40 ya mapato yanayokusanywa katika halmashauri hiyo yawe yanapelekwa kwenye kata kwa ajili ya kutekeleza miradi anayoibuliwa na wananchi.

Yahaya alitolea mfano wa stendi ya mabasi ya kata hiyo ambapo Mgalula alisema jambo hilo litapitiwa kwenye kamati ya fedha kuona namna ya kufanya na kueleza kuwa kabla ya kamti hiyo kukaa atawatuma madiwani wa viti maalumu kwenda kuangalia mradi


Zaidii

Sikiliza hapa https://www.instagram.com/reel/CzIn7V6opMS/?utm_source=ig_web_copy_link&igshid=MzRlODBiNWFlZA==

Soma hapa  https://www.michuzi.co.tz/2023/11/rais-samia-amwaga-bil-16-kutekeleza.html?m=1


Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.