• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Itigi District Council
Itigi District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
      • Maji
      • Afya
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Mji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Shera Ndogo
    • Fomu za maombi Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Taarifa kwa umma

RAIS SAMIA AMWAGA BIL 1.6/- KUTEKELEZA MIRADI ITIGI

Tarehe ya Kuwekwa: November 1st, 2023

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan amekabidhi takribani Sh.Bilioni 1.6 kwa ajili ya kukamilisha miradi ya sekta ya afya na elimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida.

Hayo yamebainishwa Oktoba 31, 2023 kupitia kikao cha robo ya kwanza cha Baraza la madiwani cha kujadili mambo mbalimbali ambacho kilikuwa na ajenda nane.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo. Hussein Simba alisema kati ya fedha hizo Sh. Milioni 700 zitatumika kununua vifaa tiba.

Alisema fedha nyingine Sh.Milioni 100 zinakwenda kujenga zahanati mbili na hivyo kuongeza idadi ya ujenzi wa zahanati hizo kufikia nane na kuwa Sh.Milioni 500 zitatumika kujenga jengo la kufulia, jengo la mionzi na dawa katika Hospitali ya Wilaya.

Simba aliongeza kuwa Sh.Milioni 180 zitatumika kwa ajili ya kuziboresha shule 10 kongwe na Sh.Milioni 128 zinakwenda kujenga bweni kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalumu.

Alisema Sh.Milioni 544 zinakwenda kujenga Shule ya Sekondari ya Majengo na zitakazosalia zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa matundu 20 ya vyoo. 

Aidha, Simba alisisitiza kwamba halmashauri hiyo imekuwa ikikusanya mara dufu zaidi ya mapato ikilinganishwa na awali ambapo mpaka sasa kiasi kilicho kusanywa kinafikia asilimia 54 na kuwa matarajio yao hadi itakapofikia robo ya tatu watafikisha asilimia 100.

Simba alipongeza juhudi za Serikali kupitia Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan namna ambayo imeonesha ushirikiano uliotukuka kwa halmashauri hiyo katika muktadha chanya wa ustawi wa maendeleo ya watu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Leila Sawe na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa wilaya hiyo, Jumanne Ismail walisisitiza halmashauri hiyo kusimamia ipasavyo matumizi ya fedha zote zinazotolewa na Serikali na wadau mbalimbali wa maendeleo.

 Naye Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, John Mgalula akizungumza kwenye kikao hicho alipokea ombi la Diwani wa Kata ya Rungwa, Said Yahaya ambaye aliomba asilimia 40 ya mapato yanayokusanywa katika halmashauri hiyo yawe yanapelekwa kwenye kata kwa ajili ya kutekeleza miradi anayoibuliwa na wananchi.

Yahaya alitolea mfano wa stendi ya mabasi ya kata hiyo ambapo Mgalula alisema jambo hilo litapitiwa kwenye kamati ya fedha kuona namna ya kufanya na kueleza kuwa kabla ya kamti hiyo kukaa atawatuma madiwani wa viti maalumu kwenda kuangalia mradi


Zaidii

Sikiliza hapa https://www.instagram.com/reel/CzIn7V6opMS/?utm_source=ig_web_copy_link&igshid=MzRlODBiNWFlZA==

Soma hapa  https://www.michuzi.co.tz/2023/11/rais-samia-amwaga-bil-16-kutekeleza.html?m=1


Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI ZA MKATABA October 17, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • TANGAZO LA KAZI ZA MKATABA October 17, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA April 08, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MAADHIMISHO SIKU YA UKIMWI

    December 10, 2024
  • SITAKI KUONA MTU ANACHEZA NA WATOTO WA SHULE-RC DENDEGO

    November 10, 2024
  • DC MANYONI APIGA MARUFUKU UKATAJI WA VICHAKA VYA ITIGI

    November 01, 2024
  • SERIKALI KUBORESHA HALI YA WAZEE

    October 17, 2024
  • Tazama zote

Video

WALIOFAULU WARIPOTI SHULENI
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Hotuba mbalimbali
  • Taarifa mbalimbali

Tuvoti mashuhuri

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

Kinasajii Watumiaji Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watumiaji

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Itigi

    Anwani ya Posta: S. L. P. 70 Itigi

    Simu: 0684483226

    Simu ya Mkononi: 0684483226

    Barua pepe: ded.itigidc@singida.go.tz

Mawasiliano Yetu

   

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • MMM
    • Ramani

Haki miliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Itigi :Haki zote zimehifadhiwa