• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

RAS MGANGA ATOA MAAGIZO

Posted on: May 12th, 2023

Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Bi .Fatma Mganga amesema namna bora ya kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendendeleo katika halmashauri ni kusimamia miradi hiyo kikamilifu ili iweze kukamilika kwa wakati na kwa viwango ili iweze kuleta tija kwa wananchi.

Akizungumza katika kikao cha robo ya tatu ya  baraza la Madiwani katika halmashauri ya Itigi RAS  amesema hakuna sababu ya miradi kushindwa kukamilika kwa wakati kwa kuwa serikali imetoa fedha za kutosha kukamilisha miradi hiyo.

Aidha ameishauri Kamati ya Fedha ,Uongozi na Mipango kuwa na Ajenda ya kupata na kujadili taarifa za miradi mbalimbali inayotekelezwa katika halmashauri kwa kila kikao ili kubaini ikiwa kuna changamoto na kuzitafutia majibu ili miradi hiyo iendelee na kukamilika kwa wakati.

Pia RAS Mganga ameitaka halmashauri kuongeza bidii katika ukusanyaji wa mapato ili kufikia lengo la asilimia 95 huku akisisitiza kuwa hali hiyo itasaidia halmashauri kujiendesha “ heshima ya halmashauri ni mapato”alisisitiza.

Katika hatua nyingine RAS ameitaka halmashauri kupitia kamati ya Elimu,Afya na Maji kuweka mikakati madhubuti kuhakikisha wanalima katika mashamba ya shule zao ili kuzalisha mazao yatakayo wawezesha kupata chakula chakula

Naye Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Kemilembe Lwota  ameipongeza halmashauri ya Itigi kwa kubuni na kuanzisha vyanzo vipya mapato ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Maegesho ya malori katika mji wa Itigi pamoja na stendi ya magari katika Kta ya Mitundu.

Pia amewakumbusha wajumbe kuanza kujiandaa kwa ajili ya mapokezi ya Mbio za mwenge wa Uhuru mnamo mwezi septemba ikiwa ni pamoja na kuhakikisha miradi yote ambayo mbio za mwenge zitapita kukagua inakamilika kwa wakati.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Itigi Mhe. Hussein Simba ameishukuru serikali inayoongozwa na Mhe,Dkt.Samia Suluhu Hassani kwa kuendelea kuipatia halmashauri hiyo fedha nyigi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na mradi mkubwa wa Hospitali ya wilaya ,miundombinu ya barabara kwa kiwango cha lami,miradi ya maji na hata elimu.

Mwisho;

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.