• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

TASAF KIPINDI CHA PILI AWAMU YA TATU HALMASHAURI YA ITIGI YAANZA NA UHAKIKI WA KAYA

Posted on: August 1st, 2020

Uwajibikaji na uadilifu kwa wataalamu ni muhimu katika kusimamia zoezi la uhakiki wa Walengwa wa kaya maskini TASAF ambao  utasaidia kupata Takwimu sahihi  za wanufaika Halisi  ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.

Kauli hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji TASAF Bi. Ester Kivuyo katika mafunzo ya Maafisa Wawezeshaji yanayohusu Utekelezaji wa kipindi cha pili cha awamu ya tatu TASAF yaliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi

Kivuyo  alisema, Lengo kuu la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo wa kiutendaji katika kusimamia Uhakiki wa kaya maskini utakaofanyika mara baada ya mafunzo hayo ili kupata Takwimu HALISI za  Walengwa HALISI ambao wamefariki (ambao walikuwa ni kaya ya mtu mmoja asiye na mtegemezi, kaya ambayo imehama, kaya ya Kiongozi wa Kijiji, kaya ya mjumbe wa Kamati ya Usimamizi ya Jamii (CMC), kaya ambayo haikufika kuchukua malipo yake  mara mbili mfululizo. Takwimu hizo zitakusanywa kwa njia ya DODOSO, na kuingizwa kwenye Mfumo wa Takwimu.

Alisema “Halmashauri ya Wilaya ya Itigi ina wanufaika  wa TASAF  3,519, kwa vijiji 39 katika kata 13 zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi ambazo zinapata huduma ya TASAF. Aliongeza kuwa Utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini pia umewezesha kaya za walengwa kujikita kwenye shughuli za kukuza kipato na kujiimarisha kiuchumi ikiwemo ufugaji, uvuvi, kilimo na biashara ndogo ndogo.

 Hata hivyo kivuyo alianisha  baadhi ya kaya za  wananchi wanaoishi katika hali duni kwenye maeneo ambayo hayakufikiwa, Hivyo Kipindi cha Pili katika Awamu ya Tatu ya TASAF  kaya zote zinazoishi katika mazingira duni zipate usaidizi wa Serikali kupitia TASAF kwa kuwawezesha kufanya kazi na kupambana na umaskini.”

 Aliongeza kuwa, Mkazo mkubwa katika Kipindi cha Pili utawekwa katika kuwezesha Kaya zitakazoandikishwa kwenye Mpango kufanya kazi ili kuongeza kipato na kuhakikisha kwamba huduma za jamii zinaongezwa na kuboreshwa  na kuendeleza rasilimali watoto hususani katika upatikanaji wa elimu na afya. 

 Aliwasisitiza  Viongozi hao kufanya kazi kwa uadilifu na weredi wakati wa utekelezaji wa Zoezi hili  kama maagizo yaliivyotolewa na Mh Rais katika hotuba  yake wakati wa uzinduzi wa Kipindi cha Pili kuhusu uwepo wa kaya hewa. “Nanukuu. “ Uwepo wa kaya hewa katika maeneo ya utekelezaji ni aibu sana kwa viongozi wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri. Nitoe wito kwa wahusika wote kusimamia vizuri mradi huu. Serikali haitakuwa na huruma kwa mtu yeyote. Kufanikiwa ama kutofanikiwa kwenye maeneo yenu itakuwa mojawapo ya vipimo nitakavyotumia kujua kama mnastahili kuendelea na nafasi mlizonazo au la. Siwatishi lakini huo ndio ukweli” mwisho wa kunukuu.

Bi Ester Kivuyo kwa kuhitimisha aliwakumbusha wananchi wote kuchukua tahadhari ya ugonjwa hatari wa COVID-19  ili   kuepuka Mikusanyiko isiyoyalazima, kuvaa barakoa,  kuepuka kushikana  mikono na  kunawa mikono kwa sabuni kwa kutumia maji safi yanayotiririka pamoja na kutumia vitakasa mikono. 

Mratibu wa Mradi wa Tasaf  Halmashauri ya Itigi ndugu Valence Kilasara (Kushoto) Akikabidhi Kishikwambi kwa Afisa Mwezeshaji Bi Haidai Magoma kwa ajili ya Uhakiki wa Kaya


Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.