• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

TUMIENI FURSA ZA MRADI WA RELI YA SGR KUINUA UCHUMI-Prof. Kahyarara Katibu Mkuu Uchukuzi

Posted on: May 15th, 2024

Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Profesa Godius Walter Kahyarara amewataka Wakazi wa Itigi Wilayani Manyoni Mkoani Singida kuwekeza katika Kilimo cha mazao ya chakula, Mbogamboga na Matunda na ufugaji wa kisasa kutokana na fursa ya mradi wa reli ya Mwendokasi ya kisasa (SGR) unaopita katika Mji wa Itigi kutoka Jijini Dar es Slaam Kuelekea Jijini Mwanza na nchi Jirani.

Prof Kahyarara amesema hayo Katika ziara yake ya kuzungumza na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kueleza fursa za kiuchumi zinzazotokana na mradi huo akiwa ameambatana na Wataalam Kutoka Wizara ya Uchukuzi, Shirikia la Reli Tanzania (TRC), Chuo Kikuu Cha Sokoine Morogoro (SUA) na Tasisi ya TanChoice Limited

Aidha ,Prof Kahyarara amesema, Serikali inaagiza mabehewa ya mizigo  yakiwa na uwezo wa kutunza ubora wa bidhaa (cold rooms) na wanajenga maghala yenye uwezo wa kutunza bidhaa (Cold rooms)  katika bandari zitakzotumika kusafirisha mizgo kwenda katika masoko duniani kote   

Prof Kahyarara amemsisitiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kuhamasisha wakulima na wafugaji kuwekeza kisasa na kupata mazao mengi ambayo watauza katika masoko ya kimataifa kwakuwa reli itakuwa ni usafiri wa uhakika , haraka na utatunza na kusafirisha bidhaa kwa ubora uleule

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Huduma  wa shirika la Reli Tanzania (TRC) Focus Makoye Sahani amesema Reli hiyo inatarajiwa kusafirisha mizigo mpaka tani 10,000 kwa mkupuo sawa na uwezo wa maroli 500 ya mizigo na inatarajiwa kutembea kwa spidi ya KM 120 kwa saa.

Aidha Sahan alisema kukamilka kwa reli hiyo kutachochea maendeleo katika sekta ya kilimo, biashara, madini na viwanda hususani katika maeneo ambapo reli hiyo inapita na kwa nchi jirani hasa Rwanda, Burundi, Uganda, Kenya na Kongo DRC

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi Ayoub Kambi alisema, Halmashauri kupitia wataalam wa Kilimo , Mifugo , biashara na ardhi wameanza kutoa elimu kwa wananchi  ili waweze kuwekeza katika mazao ya kimkakati kwa kuzingatia mahitaji ya soko

Hata hvyo Kambi, alimuelesza Katibu Mkuu kuwa kuna eneo lenye ukubwa wa hekta elfu 45 la Tanganyika Peckers katika kata ya Kiataraka ambalo lina mgogoro wa uvamizi wa wananchi ambalo linauwezo wa kuchangia uwekezaji wa mifugo na kilimo.

Hata hivyo, Kambi alisema,  jitihada za kutatua mgogoro huo zinaendelea kwa kushirikisha wananchi, Wizara ya Mifugo na Idara mbalimbali za Serikali kufikia suluhu ya mgogoro huo ili eneo hilo lianze kutumika kwa uwekezaji..

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.