• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

WAFUGAJI NYUKI HALMASHAURI YA ITIGI WAPATIWA MAFUNZO

Posted on: April 6th, 2022

        


Jamii imetakiwa kutumia fursa ya ufugaji wa nyuki kwa njia ya kitaalamu ili waweze kupata mazao mengi  na bora kwa lengo la  kujikwamua kiuchumi.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Utawala na Maendeleo ya rasilimaliwatu kutoka Idara ya Uwekezaji Viwanda na Biashara Bwana, Edward Nkembu katika mafunzo kwa wajasiriamali wanaojishughulisha na ufugaji wa nyuki katika kata za Mwamagembe,Itigi majengo na Sanjaranda katika Halmashauri ya Itigi.

Bwana Nkembu amesema kuwa mafunzo haya yamekusudiwa kuwasaidia wajasiria mali katika sekta ya nyuki kufanya shughuli zao kitaalamu ili waweze kuzalisha bidhaa  kwa wingi na zenye viwango vya ubora ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

Aidha Bw.Nkembu amesema  kuwa Idara  ya Uwekezaji ,viwanda na biashara kupitia mradi wa Enhanced Intagreted Framework(E.I.F) imepanga kuweka viwanda viwili  vya kuchakata asali pamoja na mazao yake kama nta ,maziwa ya nyuki na gundi ya nyuki katika katika kata ya Mwamagembe na Itigi majengo kutokana na maeneo hayo kuzalisha asali kwa wingi na kusisitiza kuwa mpango  huu utaongeza ajira kwa jamii “tutaweka viwanda viwili katika kata ya Mwamagembe na Itigi majengo vya kuchakata asali pamoja na mazao yake ili kuchechemua ajira pamoja na uzalishaji wenye tija katika sekta ya ufugaji wa nyuki”alisema Nkemba.

Kwa upande wake  Meneja wa SIDO  Mkoa wa Singida Bi.Agnesi Yesaya  amesema kuwa  kupitia mafunzo hayo wajasiriamali watapata maarifa  ya namna bora ya kutafuta masoko sanjari  kuhifadhi asali iliyochakatwa katika vifungashio ili kuiongezea thamani.”tunawafundisha kuongeza thamani ya mazao ya nyuki kwa  kutumia vifaa vya kisasa vya kuchakata asali na kuhifadhi katika vifungashio  bora  ili kulinda thamani ya bidhaa”amesema bi.Agnesi.

 Mkuu wa Kitengo cha Maliasili katika halmashauri ya Itigi Bwana Jonn Makotta amesema   kuwa halmashauri hiyo hukusanya mapato takribani shilingi milioni hamsini kwa mwaka kupitia tozo mbalimbali zinazotokana  na mazao ya nyuki huku akibainisha kuwa ufugaji wa nyuki una faida nyingi ikiwemo utunzaji wa mazingira.”mkifuga nyuki kisasa  mtapata mazao mengi lakini mtakuwa rafiki wa mazingira”amesema Makotta

Nao wanufaika wa mafunzo hayo Bwana Hamisi Samade wa kata ya Itigi majengo pamoja na Bi.Hadija Seif kutoka kata ya Sanjaranda wameishukuru serikali kwa kuja kuwekeza viwanda vya kuchakata asali pamoja na mazao yake katika halmashauri ya Itigi,''viwanda hivi vikikamilika vitatukomboa wajasiriamali wa ufugaji wa nyuki kwa kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja pamoja na taifa kwa ujumla'' amesema Samade.

Naye Makamu wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Itigi amesema mradi wa ujenzi wa viwanda vya kuchakata asali katika halmashauri hiyo utakaogharimu fedha takribani milioni 150  utaleta tija kwa wafugaji wa nyuki sambamba na halmashauri kwa kuwa itaweza kukusanya tozo  kutokana na uzalishaji mkubwa wa mazao hayo ya nyuki.



Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.