• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

WAFUGAJI NYUKI ITIGI DC WAUNDA JUMUIYA

Posted on: January 25th, 2023

Jumuiya mpya ya Vikundi vya Wajasiria mali wa ufugaji wa nyuki katika halmashauri ya Itigi wametakiwa kuwa na ushirikiano,umoja na nia thabiti ili jumuiya hiyo iweze kupiga hatua za kimaendeleo.

Akizungumza na wanajumuiya  kutoka vikundi 23 vinavyounda jumuiya hiyo  Mkuu wa Divisheni ya Ardhi na Maliasili Ndg. John Makotta amesisitiza kuwepo kwa umoja na ushirikiano baina yao ili waweze kujisimamia wenyewe na kuifanya  jumuiya  kuwa imara  na kwamba serikali  kupitia wizara ya maliasili na  utalii ipo tayari kutoa mafunzo ya ufugaji bora wa nyuki na biashara.ya asali na mazao yake.

Amesema kuwa serikali ina nia thabiti ya kuwainua wananchi kiuchumi  kupitia shughuli mbalimbali wanazofanya katika maeneo yao na kuongeza kuwa serikali hutoa fursa nyingi kupitia jumuiya na vikundi vilivyosajiliwa rasmi.

Nae Afisa biashara  Ndg. Emmanuel Mlenge amesema kupitia kuanzishwa kwa jumuiya hiyo wanaweza kupata fursa nyingi zikiwemo urahisi wa kupata mikopo kutoka katika taasisi za kifedha sanjari na kupata soko la uhakika la bidhaa wanazozalisha.

Pia Mlenge amewakumbusha umuhimu wa kuweka taarifa na kukmbukumbu za shughuli za kila siku zinazofanywa na jumuiya ili waweze kutambua muelekeo wa biashara ili kufikia malengo huku Mwanasheria wa halmashauri ya Itigi Ndg. Gilbart  Kalanda akiitaka jumuiya kuandaa katiba ambayo itawaongoza na kuweka muelekeo na malengo ya jumuia ambayo pia kutakuwa na sheria ndogo zitakazodhibiti ubadhilifu katika biashara ya asali na mazao yake ndani ya eneo la halmashauri.

Kwa upande wake Bwana Hamisi Samade  ambaye ni mwanajumuiya  kutoka kikundi cha ufugaji wa nyuki cha Itigi ameshukuru serikali kwa kuwaunga mkono na pia anaona kuwa jumuiya hiyo  hatimaye itakuwa  taasisi kubwa ambayo itawanufaisha wanajumuiya na jamii kwa ujumla.

Kwa upande mwingine Jumuiya  imefanya uchaguzi wa viongozi kujaza nafasi mbalimbali ambapo nafasi ya Mwenyekiti wa jumuiya  imekwenda kwa Bwana Elfasi E. Lwanji na Makamu wa Mwenyekiti ni Bi. Saada Ramadhani,Katibu wa Jumuiya ni Bw. Hamisi Samade na Katibu msaidizi ni Hamisi Ali huku nafasi ya Mweka Hazina ikichukuliwa na Bi.Wanjita  Clement.

Jumuiya ya Vikundi vya Wajasiria mali wa ufugaji wa nyuki katika halmashauri ya Itigi ambayo imepewa jina la   Jumuiya ya Wafugaji wa Nyuki Muhesi inaundwa na wanachama kutoka vikundi 23 vya wafugaji wa nyuki kutoka  Itigi,Mitundu,Kayui,Doroto,Kitaraka,Sanjaranda, Mwamagembe na Rungwa.

 

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.