• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Itigi District Council
Itigi District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara/Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
      • Maji
      • Afya
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Elimu, Afya na Mji
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Shera Ndogo
    • Fomu za maombi Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
    • Habari
    • Taarifa kwa umma

WAJUMBE WA MPDSR WAIBUKA NA MAAZIMIO

Tarehe ya Kuwekwa: May 1st, 2023

Wajumbe wa Kikao cha kujadili vifo vya akina mama vinavyotokana na uzazi pamoja na watoto wachanga (MPDSR) wameazimia kufanyia kazi changamoto mbalimbali zilizoainishwa na kujadiliwa katika kikao hicho ili kuzuia  vifo vya makundi hayo mawili.

Akifunga kikao kazi kilichofanyika katika halmashauri ya Itigi,Mganga mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Victorina Ludovick amesema vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi pamoja na vifo vya watoto wachanga vimeendelea kuongezeka katika Mkoa wa Singida vikichochewa na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na wazazi kutohudhuria kliniki au kituo cha kutolea huduma kwa wakati.

Amebainisha sababu nyingine kuwa ni pamoja na ubovu wa miundombinu ya barabara katika maeneo mengi hasa ya vijijini,uhaba wa dawa na vifaa katika vituo vya kutolea huduma sanjari na watoa huduma kushindwa kufanya maamuzi  sahihi ya kutoa rufaa kwa wakati.

Mganga Mkuu ameainisha takwimu za vifo vya akina mama na watoto wachanga kuwa tangu mwaka 2020 ni vifo 46 vya akina mama na 747 kwa watoto wachanga,2021 vifo 44 kwa akina mama na 681 kwa watoto na 2022 ni vifo 52 kwa akina mama na 540 kwa watoto wachanga na kusisitiza kuwa hali hii haikubaliki na kuongeza kuwa kikao kazi hicho kimewapa nafasi ya kuonyana,kukumbushana kuwajibika,kuboresha huduma na kuwa na takwimu sahihi.

Naye Muuguzi mkuu wa Mkoa wa Singida Hyasinta Alute ameshauri jamii ielimishwe juu ya umuhimu wa akina mama kuaza kliniki mapema ili waweze kupata huduna muhimu kwa wakati na kuongeza kuwa idara ya Afyamkoa imeendelea kushirikiana vizuri na mfumo wa M-MAMA ili kuokoa vifo vya akina mama na watoto wachanga.

Aidha Kiongozi wa timu ya Huduma Mkoba kutoka shirika la Marrie Stopes Bi. Flora Shirima ameseka kikao hiki kimeonesha maeneo ambayo yanahitaji kupewa kupaumbele na kuahidi kuwa ombi la kusaidia timu ya dharura ili kuokoa maisha ya makundi hayo mawili  ameyakariri na atayafikisha katika ngazi husika.

Kwa upande wake Meneja wa Damu salama Kanda ya kati Dkt. Kitura Mthias amesema Mkoa wa Singida umefanya vizuri katika ukusanyaji wa damu kwa asilimia 135.87 huku Mganga mkuu wa halmashauri ya Itigi Dkt. Emmanuel Mallange amewashukuru wajumbe kwa kushiriki vizuri katika kikao hicho na kusisitiza kuwa dhima ya kikao hicho ni kusema ukweli na kujifunza ili kuboresha mapungufu yanayojitokeza katika maeneo mbali mbali.

Matangazo

  • TAARIFA YA KUBATILISHA TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI LA TAREHE 17/4/2023 April 29, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI May 12, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MTUNZA KUMBUKUMBU DARAJA LA II NAFASI (3) July 27, 2022
  • TANGAZO KWA WATUMISHI WA AJIRA MPYA WALIMU NA KADA YA AFYA WALIOPANGIWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA ITIGI July 06, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • RAS MGANGA ATOA MAAGIZO

    May 12, 2023
  • SERUKAMBA KUTATUA MGOGORO ENEO LA MALISHO

    May 12, 2023
  • WAJUMBE WA MPDSR WAIBUKA NA MAAZIMIO

    May 01, 2023
  • DC.LWOTA AZINDUA MAADHIMISHO WIKI YA CHANJO ITIGI DC

    April 25, 2023
  • Tazama zote

Video

WALIOFAULU WARIPOTI SHULENI
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Hotuba mbalimbali
  • Taarifa mbalimbali

Tuvoti mashuhuri

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani

Kinasajii Watumiaji Kimataifa

world map hits counter

Idadi ya Watumiaji

writingMasterThesis

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Itigi

    Anwani ya Posta: S. L. P. 70 Itigi

    Simu: 0737235630

    Simu ya Mkononi: 0757226612

    Barua pepe: ded.itigidc@singida.go.tz

Mawasiliano Yetu

   

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • MMM
    • Ramani

Haki miliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Itigi :Haki zote zimehifadhiwa