• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Itigi District Council
Itigi District Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Itigi District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Departments/Units
      • Administration and Human Resource Management
      • Planning and Statistics
      • Finance and Trade
      • Animal Keeping and Fishing
      • Agriculture and Corperation
      • Engineering
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Community Development and Social Welfare
      • Land and Natural Resources
      • Environment and Cleaning
      • Water
      • Health
      • Information and Communication Technology
      • Election
      • Legal
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
      • Beekeeping
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Farming
    • Keeping
  • Services
    • Health
    • Water
    • Education
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
  • Councilors
    • List of Councilors
    • Committees
      • Finance
      • Education, Health and Water
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • AIDS
      • Maadili
    • Timetable
    • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • Completed Projects
  • Publications
    • Bylaws
    • Application Forms
    • Guidelines
  • Media Center
    • Videos
    • Photo Gallery
    • News
    • Press Release

WAUGUZI NI UTI WA MGONGO WA SEKTA YA AFYA

Posted on: May 28th, 2022

Serikali  imewapongeza  wauguzi nchini kwa mchango wao katika sekta ya afya kwa kuendelea kutoa huduma nzuri kwa wananchi licha ya changamoto wanazokabili.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya wauguzi  yaliyofanyika katika halmashauri ya Itigi mgeni rasmi Mganga mkuu wa halmashauri hiyo  Dkt.Emmanuel Mallange kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji Bwana  John  Mgalula amesema kuwa wauguzi wanafanya kazi kubwa  na kwa weledi katika kutoa huduma kwa jamii.

Daktari Mallange amesema kuwa bado kuna upungufu wa wauguzi katika sekta ya afya hususani ngazi ya halmashauri na kuwataka kuufanya kazi kwa juhudi na maarifa licha ya changamoto hizo na kuahidi kuwa baadhi ya changamoto na maombi ya wauguzi hao kufanyiwa kazi

Awali akisoma risala Muuguzi mkuu wa halmashauri ya Itigi Bwana Fredrick Gaisha  amebainisha baadhi ya changamoto zinzowakabili wauguzi ikiwa ni pamoja na upungufu wa wauguzi,gari ya idara ya afya  na sare za kazi huku akisisitiza kuwa kada ya wauguzi inachangia nguvukazi  ya idara ya afya kitaifa kwa asilimia sitini na zaidi ya asilimia themanini ya huduma zote za afya hutolewa na wauguzi.

Kwa upande wake Mratibu wa afya ya uzazi na watoto katika halmashauri ya Itigi Bi.Fortunata Simon amewapongeza wauguzi kwa kuchagua wito mwema na kuwataka kufanya kazi kwa upendo  ili kuokoa maisha ya watu huku Bwana Abdallah Kitunga  mkazi wa Itigi majengo aliyefika kupata huduma  za upimaji wa afya akiwapongeza wauguzi kwa kazi nzuri.

Maadhimisho ya siku ya wauguzi katika Halmashauri ya Itigi yameenda sambamba na utoaji bure wa huduma za upimaji ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi kwa akina mama,presha ,uzito,uchunguzi wa kifua kikuu,chanjo ya UVIKO-19 na kutoa elimu ya lishe juu ya makundi matano ya chakula huku kauli mbiu ikiwa ni WAUGUZI SAUTI INAYOONGOZA,WEKEZA KWENYE UUGUZI NA HESHIMU HAKI KULINDA AFYA KWA WOTE.

Announcements

  • Tangazo la kura ya Rais September 18, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI October 02, 2025
  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI October 01, 2024
  • JIMBO LA MANYONI MAGHARIBI LABADIRISHWA JINA SASA LINATAMBULIKA KAMA "JIMBO LA ITIGI" May 12, 2025
  • View All

Latest News

  • KIKAO KAZI CHA WADAU WA AFYA KUTATHIMINI TAKWIMU NA MAOTEO YA ROBO YA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2024/25

    August 27, 2025
  • MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA ITIGI KUPIIA CHAMA CHA MAPINDUZI NDG YOHANA MSITA AREJESHA FOMU YA UTEUZI WA UBUNGE

    August 27, 2025
  • TUME YA UTUMISHI WA UMMA YATOA TAARIFA YA UKAGUZI KWA MENEJIMENT YA ITIGI DC

    August 25, 2025
  • SHIMISEMITA TANGA

    August 25, 2025
  • View All

Video

YANGA DAY
More Videos

Quick Links

  • Our Instagram
  • Our Facebook
  • TAMISEMI
  • ikulu
  • NeST
  • NECTA

Related Links

  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani la Taifa
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Barabara yenye urefu wa km 10 kujengwa kwa kiwango cha lami katika mji wa Itigi kwa zaidi ya sh. bilioni 8 kukamilika julai mwakani
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap

Copyright ©2018 Itigi Distict Council. All rights reserved.